Azam Fc ni mwendo wa vipigo Ligi Kuu

Joel JJ By Joel JJ β€’ 22nd December 2023


Azam Fc ni mwendo wa vipigo Ligi Kuu

Timu ya Azam imeendelea kujikita kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu Bara baada ya jana kuendeleza wimbi la ushindi wakiichapa Kagera Sugar mabao 4-0 katika mchezo uliopigwa Uwanja wa Kaitaba, Bukoba

Mabao ya Azam yalifungwa na Feisal Salum 'Fei Toto' dakika ya '9, Prince Dube dakika ya 11, Pascal Msindo dakika ya 45 na Alassane Diao dakika ya 84 na kuifanya timu hiyo kufikisha jumla ya pointi 31 katika michezo 13 iliyocheza hadi sasa

Pointi hizo 31 ilizonazo Azam zinaifanya kuendelea kujikita kileleni na kuiacha Yanga ambao ni mabingwa watetezi wa taji hilo ikiwa na 27 ingawa imecheza michezo 10 ambayo ni mitatu pungufu ya vinara hao kwa sasa wa Ligi Kuu Bara msimu huu

Baada ya kufunga bao katika mchezo huo, Fei Toto amefikisha jumla ya mabao manane ya Ligi Kuu Bara akiwa na kikosi hicho msimu huu akipitwa moja tu na kinara wa Yanga, Stephane Aziz KI anayeongoza akiwa amefunga tisa

Ushindi wa Azam unaifanya timu hiyo kufikisha jumla ya michezo sita mfululizo ya Ligi Kuu Bara bila ya kupoteza tangu mara ya mwisho ilipofungwa mabao 3-1, dhidi ya Namungo Oktoba 27, mwaka huu kwenye uwanja wake wa Azam Complex, Chamazi


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.