Bodi ya Ligi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), imeufungia uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam kutumika kwa michezo ya Ligi kwa kukosa vigezo vya kikanuni na sheria za mpira wa miguu
Miundombinu ya uwanja huo haikidhi matakwa ya Kanuni kama ilivyoainishwa kwenye masharti ya Kanuni ya Leseni za Klabu
Kufuatia uamuzi huo, timu zote zinazotumia uwanja huo kwa michezo yao ya nyumbani zitalazimika kutumia uwanja mwingine kama Kanuni inavyoelekeza mpaka uwanja wao utakapofunguliwa, baada ya kufanyiwa marekebisho na kukaguliwa na TFF
Simba na KMC zinazotumia uwanja huo zitalazimika kutafuta viwanja vingine kwa mechi zao za nyumbani



