Phiri mikononi mwa Benchikha

Joel JJ By Joel JJ β€’ 25th December 2023


Phiri mikononi mwa Benchikha

Licha ya kuwepo kwa tetesi za mshambuliaji Moses Phiri kuandika barua ya kuomba kuvunja mkataba wake kutokana na kukosa nafasi kwenye kikosi cha kwanza, hatma yake imebaki mikononi mwa kocha Abdelhak Benchikha

Phiri mmoja wa wachezaji ambao Wanamsimbazi walikuwa na matumaini makubwa kwake, imekuwa si rahisi kwake kupata nafasi ya kudumu kwenye kikosi cha kwanza tangu wakati Simba ikinolewa na Robertinho Oliveira

Nyota huyo kutoka Zambia ambaye msimu huu amefunga mabao matatu, pia amekosa nafasi katika mechi za mwanzo za kocha wa sasa, Benchikha

Hata hivyo taarifa kutoka ndani ya uongozi wa Simba imebainisha kuwa, hatma yake itategemea na ripoti ya Benchikha ambayo wataifanyia kazi katika dirisha hili dogo la usajili ambalo litafungwa Januari 15 2024

Inafahamika Phiri anahusishwa na Yanga hivyo hata ikitokea Simba itaamua kuachana nae, lazima makubaliano hayo yatahakikisha haendi upande wa pili katika dirisha hili

Nyota huyo alisajiliwa na Simba msimu uliopita kutoka Zanaco baada ya mabosi wa Msimbazi kuwazidi Yanga waliokuwa wakimpigia hesabu na kumfuata hadi Zambia ili kumshawishi

Phiri alikuwa na wakati mzuri chini ya kocha Juma Mgunda akiibeba Simba Ligi ya Mabingwa msimu uliopita na kwenye ligi kabla ya kuumia na kukaa nje kwa muda mrefu, hadi alipoingia Robertinho.


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.