Baada ya kufanyiwa ukarabati mkubwa, Uwanja wa Amaan Visiwani Zanzibar ambao utatumika katika michuano ya kombe la Mapinduzi, utazinduliwa leo Jumatano
Mchezo wa kirafiki kati ya timu ya Taifa ya Tanzania Bara (Kilimanjaro Stars) dhidi ya timu ya Taifa ya Zanzibar (Zanzibar Heroes), utapigwa katika uwanja huo
Mchezo huo ambao hautakuwa na kiingilio utapigwa saa 2:15 Usiku
Maboresho ya Uwanja wa Amaan yamefuata mahitaji yote ya CAF na FIFA hivyo uwanja huo utaweza kutumika hata katika michuano ya Kimataifa inayoandaliwa na CAF/FIFA







