Tanzania - Taifa Stars - Yanga - Simba - Azam - Local

SMZ kujenga viwanja zaidi Zanzibar

Joel JJ By Joel JJ
β€’
28 Dec 2023
SMZ kujenga viwanja zaidi Zanzibar

Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Dr. Ali Hassan Mwinyi amesema serikali yake ipo katika mpango wa ujenzi wa viwanja vingine vya mpira huku akiahidi michuano ya Afcon 2027 itafanyika katika uwanja huo mpya 

Rais Mwinyi aliyasema hayo jana katika uzinduzi wa uwanja wa Amaan baada ya ukarabati mkubwa. Uzinduzi huo ulikwenda sambamba na mchezo wa kirafiki kati ya Zanzibar Heroes dhidi ya Kilimanjaro Stars uliomalizika kwa suluhu ya bila kufungana

Aidha, Rais Dk.Mwinyi ameeleza kuwa Serikali imelenga kujenga miundombinu ya michezo kila wilaya kwa viwanja vipya vya kisasa

Vilevile Rais Dk.Mwinyi amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Serikali ya Ujerumani kupitia shirika la maendeleo GIZ imefunga mkataba wa makubaliano kwa ajili ya ujenzi wa viwanja vitano vya michezo midogomidogo ikiwemo mpira wa kikapu, mpira wa wavu , mpira wa mikono na mpira wa pete

Viwanja hivyo vinatarajiwa kujengwa Kangani Wilaya ya Mkoani, Mchangamdogo Wilaya ya Wete, Tumbatu na Mkokotoni Wilaya ya Kaskazini A na Haile Selasie Wilaya ya Mjini pamoja na viwanja vitatu vya Tennis Chakechake, Chuo kikuu cha SUZA Kampasi ya Nkurumah na Skuli ya Regeza Mwendo katika Wilaya ya Magharibi B

Halikadhalika Serikali ya Zanzibar imefanikiwa kuwapeleka vijana katika nchi mbalimbali ikiwemo Uturuki na Afrika Kusini kwa lengo la kuendelezwa na baadae kucheza soka la kulipwa.

Rais Dk.Mwinyi amewahimiza wananchi kushiriki Tamasha la kila mwaka la mazoezi linalofanyika tarehe Mosi ya mwaka mpya.

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
45m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
2h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
4h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’