Meneja wa Habari na Mawasiliano klabu ya Simba Ahmed Ally amewatoka hofu wanachama na mashabiki wa timu hiyo juu ya michakato ya usajili katika dirisha dogo lililofunguliwa Disemba 16 likitarajiwa kufungwa Januari 15 2024
Ahmed amesema michakato ya usajili inaendelea na mpaka sasa kuna wachezaji ambao tayari wamesajiliwa kinachosubiriwa ni utambulisho wao tu
"Wanasimba wasidhani tuko kimya, kuna mambo makubwa yanafanyika nyuma ya pazia. Safari huu tunaleta wachezaji ambao wameiva, sio wachezaji wa kusubiri kwani muda huo haupo"
"Tetesi zimekuwa nyingi lakini muhimu Wanasimba wasubiri taarifa rasmi kutoka katika vyanzo vyetu vya habari"
"Wanasema kimya kingi kina mshindo mkubwa, kuna usajili umefanyika huo utakwenda kujaza maji kwenye mabwawa yote ya kuzalisha umeme na kumaliza kabisa tatizo la mgao wa umeme," alitamba Ahmed
Taarifa za ndani ya uongozi wa Simba zimedokeza kuwa takribani wachezaji watano au sita wataongezwa katika dirisha hili dogo



