Mabingwa wa soka Tanzania Bara Yanga leo wanatupa karata yao ya kwanza katika michuano ya kombe la Mapinduzi kwa mchezo dhidi ya Jamhuri ambao utapigwa saa 2:15 usiku katika uwanja wa New Amaan Complex
Wananchi walitua Zanzibar jana wakiwa na msafara uliojumuisha wachezaji 22
Kocha Miguel Gamondi aliongoza kikosi jana jioni katika mazoezi ya mwisho yaliyofanyika uwanja wa Amaan
Ukiangalia benchi la ufundi limekamilika, wachezaji wote ambao hawako kwenye majukumu ya timu za Taifa wamesafiri isipo kuwa Yao Kouassi na Khalid Aucho ambao imeelezwa wana ruhusa maalum
Meneja wa Habari na Mawasiliano klabu ya Yanga Ali Kamwe amesema wanataka kutwaa taji la Mapinduzi msimu huu
Aidha Kamwe amewataka mashabiki wa Yanga kuhakikisha wanawahi mapema uwanja wa Amaan kwani kabla ya mchezo kutakuwa na utambulisho wa mchezaji mpya