Simba imepata tiba eneo la kiungo

Joel JJ By Joel JJ β€’ 7th January 2024


Simba imepata tiba eneo la kiungo

Mapema Jumamosi, Simba ilitambulisha usajili wa kiungo mkabaji Babacar Sarr raia wa Senegal. Sarr amewahi kuitumikia klabu ya US Monastir ya Tunisia

Sarr anayetumia zaidi mguu wa kulia, mwenye umri wa miaka 26, ametua Simba kwa mkataba wa miaka miwili

Uzoefu pamoja na uwezo wake wa kutawala eneo la kiungo cha ukabaji imetajwa kuwa sababu kuu iliyoishawishi Simba kumleta Msimbazi

Mbali na kuitumikia US Monastir ambayo msimu uliopita ilicheza robo fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika, Sarr pia amewahi kuzichezea Olympique Beja ya Tunisia, Teungueth FC, AS Pikine na Mbour P.C.

Sarr ameungana na Fabrice Ngoma, Sadio Kanoute na Mzamiru Yassin ambapo saa ameongeza wigo katika eneo la kiungo

Bila shaka sasa Sarr anakuja kumaliza changamoto katika eneo hilo


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.