Mapema Jumamosi, Simba ilitambulisha usajili wa kiungo mkabaji Babacar Sarr raia wa Senegal. Sarr amewahi kuitumikia klabu ya US Monastir ya Tunisia
Sarr anayetumia zaidi mguu wa kulia, mwenye umri wa miaka 26, ametua Simba kwa mkataba wa miaka miwili
Uzoefu pamoja na uwezo wake wa kutawala eneo la kiungo cha ukabaji imetajwa kuwa sababu kuu iliyoishawishi Simba kumleta Msimbazi
Mbali na kuitumikia US Monastir ambayo msimu uliopita ilicheza robo fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika, Sarr pia amewahi kuzichezea Olympique Beja ya Tunisia, Teungueth FC, AS Pikine na Mbour P.C.
Sarr ameungana na Fabrice Ngoma, Sadio Kanoute na Mzamiru Yassin ambapo saa ameongeza wigo katika eneo la kiungo
Bila shaka sasa Sarr anakuja kumaliza changamoto katika eneo hilo



