Michuano ya Afcon 2023 inaendelea huko Ivory Coast ambapo leo timu ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' itatupa karata yake ya kwanza katika michuano hiyo kwa kumenyana na Morocco katika mchezo utakaopigwa saa 2 usiku
Leo ni mechi mbili tu zitapigwa kundi F ambapo mchezo mwingine ni kati ya Zambia dhidi ya DR Congo ambao utapigwa saa 5 usiku
Michuano ya Afcon mwaka huu imeendelea kutoa matokeo yasiyotarajiwa baadhi ya mechi ambapo timu vigogo zimeshindwa kuondoka na alama zote tatu
Ni wazi hautakuwa mchezo mwepesi kwa Stars dhidi ya Morocco iliyokamilika sawasawa lakini hakuna lisilowezekana katika mpira wa miguu
Kocha Mkuu wa Stars Adel Amrouche amesema wanafahamu wana mtihani mgumu mbele ya Morocco lakini hawakwenda Ivory Coast kutalii hivyo watapambana



