Yanga - Local

Gamondi ampa masharti Okrah

Joel JJ By Joel JJ
19 Jan 2024
Gamondi ampa masharti Okrah

Kocha Mkuu wa Yanga Miguel Gamondi ameeleza kufurahishwa na usajili wa kiungo mshambuali Augustine Okrah akibainisha kuwa mchezaji huyo atakuwa na mchango katika kikosi chake

Hata hivyo Gamondi amesisitiza ni lazima apambane kwenye kiwanja cha mazoezi ili kujihakikishia nafasi ya kucheza

Okrah alisajiliwa na Yanga katika dirisha dogo akitokea klabu ya Bechem United ya kwao Ghana

Ni mmoja wa wachezaji watatu waliosajiliwa kwenye dirisha dogo wengine wakiwa Shekhan Khamis na Joseph Guede

"Nimemuona Okrah ni mchezaji mzuri naamini ataongeza kitu katika eneo letu la ushambuliaji. Hata hivyo ni lazima apambane katika kiwanja cha mazoezi kwani utaratibu wetu hapa tunatoa nafasi kwa mchezaji anayefanya vizuri mazoezini kwani kile tunachokifanya mazoezini ndicho tunakifanya kwenye mechi," alisema Gamondi

Nae Okrah amesema anatambua amejiunga katika timu bora yenye wachezaji mahiri hivyo atahakikisha anatimiza vyema majukumu yake ili awe msaada kwa timu

"Natambua ubora wa kila mchezaji wa Yanga hususan maeneo ninayocheza, hilo linanifanya kuungana nao na kufanya vyema kwa ajili ya manufaa ya timu pia inanipa ari ya kupambana zaidi ili kupata nafasi kikosini"

"Mimi sio mgeni hapa Tanzania, nimewahi kucheza Simba na sasa nimerudi nikiwa na Yanga nadhani tutakuwa na safu bora zaidi ya ushambuliaji," alisema

More Stories

SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa  Yanga SC “Your next: Yanga”
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa Yanga SC “Your next: Yanga”
1m ago
READ MORE →
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
1h ago
READ MORE →
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
11h ago
READ MORE →
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
12h ago
READ MORE →
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
12h ago
READ MORE →
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
16h ago
READ MORE →
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
19h ago
READ MORE →
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
20h ago
READ MORE →
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
20h ago
READ MORE →
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
21h ago
READ MORE →