Tanzania - Taifa Stars - Yanga - Simba - Azam - Local

Amrouche bado ni kocha wa Stars

Joel JJ By Joel JJ
β€’
23 Jan 2024
Amrouche bado ni kocha wa Stars

Licha ya kuwepo taarifa za kufutwa kazi kwa Kocha Mkuu wa kikosi cha timu ya Taifa Tanzania ‘Taifa Stars’ Adel Amrouche, lakini Waziri wa Sanaa, Utamaduni na Michezo, Dkt. Damas Ndumbaro ameweka wazi kuwa kocha huyo yuko sana katika kikosi cha Stars

Waziri huyo amesema Serikali iko pamoja na kocha huyo hata pale adhabu yake ya kufungiwa mechi nane na Shirikisho la Soka Afrika (CAF) itakapomalizika

Dkt. Ndumbaro amesema kuwa kocha huyo raia wa Algeria amefanya makubwa na ndiye aliyeifikisha timu kwenye michuano ya AFCON inayoendelea huko nchini Ivory Coast, hivyo watakuwa nae katika changamoto anazopitia na hawatasitisha mkataba wake

"Bado sisi kama Serikali ambao ndiyo walipa mshahara ukiadhibiwa sio muda wa kumzodoa, tupo naye kwenye kipindi hiki kigumu anachopitia"

"Bado tuna imani nae, yeye ndiye aliyetufikisha hapa sehemu ya kufuzu. Mwalimu huyu ndiye ametengeneza timu hii, tupo na mwalimu, hatujasitisha mkataba, ameadhibiwa na CAF, hajaadhibiwa na serikali wala TFF"

"Sisi katika kipindi hiki kigumu ambacho mwalimu ana kipitia tuko nae na tutaendelea kuwa nae, kumpa sapoti yote ambayo inahitajika, ili yeye apite kwenye kipindi hiki kigumu kwa salama kabisa" alisema Dkt. Ndumbaro

Baada ya kocha huyo kufungiwa, kikosi hicho kwa sasa kipo chini ya makocha wa muda Hemed Suleiman na Juma Mgunda

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
5h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
5h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
5h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
9h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
12h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
13h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
13h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
14h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
15h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
16h ago
READ MORE β†’