Baada ya kuondoshwa mapema katika michuano ya Afcon, timu ya Taifa ya Algeria inasaka kocha mpya baada ya kumtimua Djamel Belmadi
Kocha Mkuu wa Simba Abdelhak Benchikha ni miongoni mwa makocha ambao taarifa zinaeleza amependekezwa kumrith Belmadi
Benchikha anatizamwa kama kocha mwenye mafanikio zaidi nchini Algeria katika misimu ya karibuni wakiamini anaweza kurejesha nidhamu ya mabingwa hao wa Afcon 2019
Hata hivyoBenchikha amegomea ofa hiyo akihitaji kuhudumia mkataba wake na Simba ambao ndio kwanza una takribani miezi miwili tu
Benchikha amepania kufanya mambo makubwa na Simba jukumu lake la kwanza likiwa kuivusha Simba hatua ya makundi michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika
Simba ilimchukua Benchikha baada ya kuachana na Robertinho Oliveira. Benchikha aliachana na USM Alger aliyoipa mafanikio makubwa msimu uliopita kwa kushinda mataji ya CAF CC na CAF Super Cup