Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limeikubalia timu ya Singida Fontain Gate kutumia Uwanja wa CCM Kirumba kuwa wa nyumbani baada ya uwanja iliokuwa inatumia awali kuufungia
Kutokana na timu hiyo kuutumia uwanja huo kuanzia sasa, huenda mechi za Singida Fountain Gate za nyumbani dhidi ya Simba na Yanga zikachezwa jijini Mwanza kulingana na ratiba ya michezo husika
Awali, Singida Fountain Gate ilikuwa inatumia Uwanja wa CCM Liti, lakini imefungiwa kutokana na kutokidhi viwango vinavyohitajika
Viongozi wa timu hiyo walipeleka maombi ya kutumia Uwanja wa CCM Kirumba kwa mechi zilizobaki - ombi lao limekubaliwa
"Tutatumia uwanja huo kwa mechi zote za nyumbani. Tunashukuru kwa maombi hayo kukubaliwa," msemaji wa Singida FG alithibitisha