Derby ya Mzizima inapigwa jijini Mwanza leo, wenyeji Simba wakiwakaribisha Azam Fc katika mchezo wa ligi kuu ya NBC
Hii ni mechi muhimu sana kwa kila timu kuvuna alama tatu ili kujiweka katika nafasi nzuri kwenye mbio za ubingwa wa ligi kuu msimu huu
Msimu huu Azam Fc wanaonekana kuwa washindani wa kweli katika mbio za ubingwa, ushindi katika mchezo huu utaendelea kuwawekaa katika nafasi nzuri katika mbio za ubingwa wakiendelea kuipa presha Yanga iliyo kileleni
Kwa Simba, ushindi utawahakikishia kuinondoa Azam Fc katika nafasi ya pili huku pia wakiendelea kuwa na mechi ya kiporo ambayo kama watashinda tofauti yao na vinara Yanga itakuwa alama mbili tu
Katika misimu ya karibuni, Azam Fc wameonekana kuimudu Simba wakipata matokeo mazuri katika mechi zilizokutanisha timu hizo
Msimu uliopita Simba haikuweza kupata ushindi katika mechi zote walizokutana na Azam Fc kwenye ligi na kombe la FA
Baada ya ushindi katika mechi tatu zilizopita, Simba inakwenda kwenye mchezo huo ikiwa katika wakati mzuri zaidi kuliko wapinzani wao ambao huu utakuwa mchezo wao wa kwanza tangu ligi iliporejea
Ni katika uwanja wa CCM Kirumba, saa 10 jioni