Yanga - Local

Yanga vs CR Belouizdad ni mechi ya kisasi

Joel JJ By Joel JJ
β€’
19 Feb 2024
Yanga vs CR Belouizdad ni mechi ya kisasi

Baada ya ushindi mnono wa mabao 3-0 dhidi ya KMC katika mchezo wa ligi kuu uliopigwa mkoani Morogoro, Wananchi sasa wanaelekeza nguvu zao kwenye michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika

Ni Jumamosi ya Februari 24, Yanga itakuwa mwenyeji wa CR Belouizdad katika mchezo wa raundi ya tano kundi D utakaopigwa uwanja wa Benjamin Mkapa saa 1 usiku

Hii ni kama fainali kwa Yanga kwani Wananchi wanahitaji ushindi ili kujiweka katika nafasi nzuri ya kutinga robo fainali

Yanga itaingia katika mchezo huu ikiwa na kumbukumbu ya kupoteza kwa mabao 3-0 katika mchezo wa kwanza ulioipigwa Algeria

Hivyo hii ni mechi ya kisasi, deni inapaswa lilipwe mbele ya mashabiki 60,000 ambao wanatarajiwa kujitokeza kuishangilia Yanga

Aidha ushindi wa zaidi ya mabao 3 unaweza kutosha kuipeleka Yanga robo fainali hasa kama itatokea Medeama watakosa ushindi dhidi ya Al Ahly katika mchezo utakaopigwa Februari 23 huko Ghana

Katika msimamo wa kundi D, Al Ahly wako kileleni wakiwa na alama sita, Belouizdad iko nafasi ya pili ikiwa na alama tano sawa na Yanga timu hizo zikitofautiana mabao

Medeama wako nafasi ya nne wakiwa na alama nne. KIla timu kundi D ina nafasi ya kwenda robo fainali

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
1h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
2h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
3h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
5h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
19h ago
READ MORE β†’