Ihefu - Geita - Local

Tchakei, Rupia warejesha makali ya Ihefu Fc

Joel JJ By Joel JJ
β€’
19 Feb 2024
Tchakei, Rupia warejesha makali ya Ihefu Fc

Ihefu Fc meendelea kutoa vichapo kwa wapinzani Ligi Kuu baada ya usajili mkubwa walioufanya kwenye dirisha dogo kwa kuwaleta mastaa kibao akiwemo mshambuliaji, Elvis Rupia na kiungo Marouf Tchakei ambao wameendelea kuibeba katika michezo ya Ligi Kuu

Baada ya kuipa Ihefu ushindi 3-2 kwenye mchezo uliopita dhidi ya Mtibwa Sugar, nyota hao leo wameifungia mabao muhimu timu hiyo na kuiwezesha kuondoka na ushindi wa mabao 2-1 ugenini mbele ya Geita Gold kwenye Uwanja wa Nyankumbu, mjini Geita, ukiwa ni ushindi wa pili mfululizo

Rupia aliitanguliza timu yake mapema katika dakika ya tano kwa kichwa akiunganisha krosi ya Marouf Tchakei, kabla ya Tchakei naye kuweka chuma cha pili katika dakika ya 12 akimalizia pasi ya Hernest Malonga na kwenda mapumziko wikiwa kifua mbele kwa mabao 2-0

Baada ya kufunga leo katika mchezo huo ambao ulianza saa 8:00 mchana, Tchakei anafikisha bao lake la saba kwenye Ligi Kuu, huku Rupia akifikisha bao la tatu

Geita Gold imekubali kichapo cha kwanza nyumbani kwenye Uwanja wa Nyankumbu tangu Septemba 30, 2023 ilipofungwa mabao 2-1 na KMC, ambapo baada ya hapo ilicheza mechi tano dimbani hapo bila kupoteza ikishinda tatu na sare mbili

Ihefu imelipa kisasi cha kufungwa bao 1-0 katika mzunguko wa kwanza mchezo uliopigwa Agosti 15, 2023 kwenye Uwanja wa Highland Estates, Mbeya.

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
45m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
2h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
4h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’