Raia wawili kutoka Tanzania maarufu kama Ramadhani Brothers, wameibuka washindi katika shindano la kusaka vipaji la America’s Got Talent (AGT) Fantasy-Legue na kujinyakulia kitita cha dola 250,000 (Sh637 milioni)
Ndugu hao, Fadhili Ramadhani na Ibrahim Job, waliwashinda washindani wengine tisa waliofika fainali - wawili kati yao walikuwa wakichuana na timu ya Howie na waliobaki kwenye timu za majaji Simon Cowell, Mel B na Heidi Klum
"Kushinda AGT: Ligi ya Ndoto ni hisia ya kushangaza zaidi ambayo hatuwezi kuelezea!" alisema Fadhili baada ya kutangazwa washindi
"Tumekuwa katika mashindano mengine ya Got Talent duniani kote na tumefika kila fainali, lakini hatujawahi kushinda. Lakini kushinda dhidi ya washindi wa zamani wa AGT ni baadhi ya vitendo bora zaidi kwenye sayari, kwa kweli kunainua hadhi yetu"
Ndugu hao ambao hutumia balansi ya mikono na kichwa, kwa mara ya kwanza walishiriki AGT msimu wa 18 mwaka wa 2023, lakini walimaliza katika nafasi ya tano licha ya matukio yao ya kusisimua.