Pacome Day iliyozinduliwa juzi na Yanga imezidi kuwa kubwa baada ya Bank ya CRDB kuweka fedha kudhamini tukio hilo ambalo kilele chake ni Jumamosi Februari 24 katika mchezo wa ligi ya mabingwa kati ya Yanga dhidi ya CR Belouizdad ambao utapigwa uwanja wa Benjamin Mkapa
Meneja wa Habari na Mawasiliano klabu ya Yanga Ali Kamwe ameipongeza CRBD kwa kuona umuhimu wa kudhamini tukio hilo ambalo ni mwendelezo wa ubunifu unaofanywa na Idara ya Habari na Mawasiliano
"Ninayo furaha kubwa kuwatangazia Wananchi kuwa Wiki ya Hamasa ya Pacome Day”imedhaminiwa na Benki Bora Tanzania ya CRDB"
"CRDB wametoa Fedha ya kutosha kudhamini 'Pacome Day’' Ilianza kwa Taasisi za ZIPPA na ZRA kwa kuidhamini BACCA DAY na sasa PACOME DAY imetupa pia mpunga Wananchi"
"Haya mambo hayatokei bahati mbaya. Ni matokeo ya Ubunifu mkubwa kutoka kwa Watendaji wa Yanga unaowaunganisha Mashabiki na Wanachama wake kwenye Hamasa Nchi nzima," alisema Kamwe
Mashabiki wa Yanga wameaswa kuendelea kununua tiketi ili kuhakikisha siku ya Jumamosi uwanja wa Benjamin Mkapa unajaa



