Yanga imetinga robo fainali ya michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika baada ya ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya CR Belouizdad
Hii ni historia mpya kwa Yanga kufanikiwa kutinga robo fainali ya ligi ya mabingwa tena kwa ushindi mnono
Mudathir Yahya aliipeleka Yanga mapumziko ikiwa mbele kwa bao 1-0 akimalizia krosi ya Joyce Lomalisa
Kipindi cha pili Yanga ilirejea kwa kasi na kufunga mabao mawili haraka dakika ya 47 na 48 kupitia kwa Stephane Aziz Ki na Kennedy Musoma
Pengine Aziz Ki angeongeza bao jingine kama angetumia vyema moja ya nafasi adimu lakini alisahihisha makosa yake kwa kumtengenezea Joseph Guede nafasi ya kufunga bao la nne
Yanga inatinga robo fainali baada ya kufikisha alama 8 huku ikiwa na faida ya head-to-head dhidi ya CR Belouizdad
Hii ina maana hata Belouizdad washinde mabao 100 katika mechi yao ya mwisho na Yanga ikafungwa mabao 1000 na Al Ahly, bado itabaki nafasi ya pili
Mechi ya mwisho dhidi ya Al Ahly itakuwa vita ya kuamua timu itakayomaliza nafasi ya kwanza