Kiungo wa kati wa Chelsea Conor Gallagher anataka kusalia Stamford Bridge. Mchezaji huyo wa kimataifa wa Uingereza mwenye umri wa miaka 24 amebakiza miezi 18 katika mkataba wake na amekuwa akihusishwa na kuhamia Tottenham. (Sky Sports)
Arsenal inamfuatilia mshambuliaji wa Brighton na Jamhuri ya Ireland Evan Ferguson, 19, huku wakipania kuimarisha safu yao ya ushambuliaji msimu wa joto. (Football Insider)
Mkurugenzi wa michezo wa Arsenal Edu anasema klabu hiyo "tayari ina malengo yetu" alipoulizwa kuhusu The Gunners kusajili mshambuliaji mpya. (TNT Sports, via Standard)
Mshambulizi wa Napoli Victor Osimhen anaweza kuwa chaguo kwa Arsenal lakini wanakabiliwa na ushindani kutoka kwa Chelsea na Paris St-Germain kumnunua mchezaji huyo wa kimataifa wa Nigeria mwenye umri wa miaka 25. (GiveMeSport)
Kiungo wa kati wa Uingereza Jack Harrison, 27, anataka kubadilisha uhamisho wake wa mkopo kutoka Leeds United hadi Everton kuwa mkataba wa kudumu msimu huu wa joto hata kama timu hiyo ya Elland Road itapandishwa daraja na kurejea Ligi Kuu ya Uingereza. (Football Insider)
Mwekezaji mpya wa Manchester United Sir Jim Ratcliffe anataka mfumo mpya wa malipo utambulishwe katika klabu hiyo, huku mishahara ya wachezaji ikitegemea zaidi mafanikio. (Mirror)
Manchester United wanalenga kusajili mshambuliaji, mabeki wawili wakati wa marekebisho ya kikosi cha klabu hiyo ya Old Trafford majira ya kiangazi. (Telegraph - usajili unahitajika)
Juventus wameweka bei ya pauni milioni 51 kumnunua Kenan Yildiz anayewindwa na Arsenal. Mshambulizi huyo mwenye umri wa miaka 18 amecheza mechi 15 pekee akiwa na Juventus tangu ajiunge na klabu hiyo akitokea Bayern Munich mwaka wa 2022. (Sun)
Mshambuliaji wa Brazil Endrick anatazamiwa kujiunga na Real Madrid atakapofikisha umri wa miaka 18 mwezi Julai, lakini Palmeiras wanajaribu kumbakisha hadi Desemba. (ESPN)
BBC



