Barcelona bado wanavutiwa na kocha wa Arsenal Mikel Arteta kuchukua nafasi ya Xavi, ambaye anaondoka mwishoni mwa msimu huu, lakini klabu hiyo ya Uhispania inajua itakuwa vigumu kumteua. (Relevo)
Kocha wa England Gareth Southgate na mkufunzi wa Brentford Thomas Frank ni miongoni mwa chaguzi zinazozingatiwa na Manchester United ikiwa watachagua kuchukua nafasi ya Erik ten Hag mwishoni mwa msimu huu. (ESPN)
Liverpool, Arsenal na Manchester City wanapigana vikumbo kumsajili kiungo wa Bayern Munich Joshua Kimmich. Mchezaji huyo wa kimataifa wa Ujerumani mwenye umri wa miaka 29 anatazamia kuondoka Bavaria msimu huu wa joto. (Express)
Klabu yoyote inayotaka kumwajiri kocha mkuu wa Brighton Roberto de Zerbi msimu huu wa joto italazimika kuwalipa Seagulls £12.8m. Barcelona, Liverpool na Manchester United wamehusishwa na Muitaliano huyo. (Mirror)
Bayern Munich wako mbele ya Liverpool katika kinyang'anyiro cha kumteua Xabi Alonso kama kocha wao mwingine ikiwa Muhispania huyo ataamua kuondoka Bayer Leverkusen msimu wa joto. (Telegraph)
Liverpool wana nia ya kumteua Richard Hughes kama mkurugenzi wa michezo baada ya yeye mwenyewe 44, kuthibitisha kuwa ataacha nafasi yake kama mkurugenzi wa kiufundi wa Bournemouth mwishoni mwa msimu huu. (Times)
Liverpool, Borussia Dortmund na Paris St-Germain wanamtaka kiungo wa kati wa Argentina Alan Varela, 22, lakini watalazimika kulipa Porto kifungu chake cha pauni milioni 60. (Mercato)
Kiungo wa kati wa Brazil Joelinton anataka kusalia katika Ligi ya Premia ikiwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27 hatakubali mkataba mpya zaidi ya 2025 na Newcastle United. (Football Insider)
Chelsea wanataka kumsajili winga wa Athletic Bilbao Nico Williams. Mshambuliaji huyo wa Uhispania mwenye umri wa miaka 21 ana kipengele cha kutolewa ambacho kinaweza kumaanisha kuwa anapatikana kwa pauni milioni 43 msimu huu wa joto. (Telegraph)
Williams pia yuko kwenye rada za Arsenal huku winga wa Wolves Mreno Pedro Neto mwenye umri wa miaka 23 na mshambuliaji wa Brentford Ivan Toney, 27, wakizingatiwa pia. (Evening Standard)
West Ham wamepewa nafasi ya kumsajili winga wa Borussia Dortmund Mjerumani Marco Reus, 34, mkataba wake utakapokamilika msimu huu wa joto. (Football Insider) Kiungo wa kati wa Ajax Jordan Henderson, 33, hajutii kuondoka Liverpool, akisema ulikuwa "uamuzi bora" kwa pande zote. (Guardian)
BBC



