KMC - Tabora - Local

Waziri Junior aongeza hat-trik Ligi Kuu

Joel JJ By Joel JJ
11 Mar 2024
Waziri Junior aongeza hat-trik Ligi Kuu

Mshambuliaji wa KMC, Wazir Junior jana alionyesha umwamba wake baada ya kutupia ‘hat trick’ timu yake ilipoichapa Tabora United mabao 4-2, kwenye Uwanja wa Azam Complex Chamazi

Hii ni hat trick ya tano kwenye Ligi Kuu Bara msimu huu, baada ya nyingine za awali kufungwa na Feisal Salum 'Fei Toto' wa Azam, Jean Baleke akiwa na Simba, Stephen Aziz Ki Yanga na Kipre Junior Azam.

Hata hivyo, Tabora imeweka rekodi ya wachezaji wawili kufunga ‘hat trick’ dhidi yake baada ya awali Fei Toto kufanya hivyo kwenye mchezo wa kwanza kabisa wa Ligi Kuu.

Junior alitumia dakika 20 tu kufunga hat trick yake ya kwanza msimu huu baada ya kufunga katika dakika za 49, 60 na 67 na kuwa mzawa wa pili aliyefunga idadi hiyo ya mabao kwenye mchezo mmoja wa ligi msimu huu.

Sasa staa huyo amesogea hadi nafasi ya pili kwenye chati ya ufungaji akifunga mabao 11 sawa na Aziz Ki, lakini akiwa bao moja nyuma ya kinara wa mabao kwa sasa, Fei Toto mwenye 12.

More Stories

SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa  Yanga SC “Your next: Yanga”
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa Yanga SC “Your next: Yanga”
1m ago
READ MORE →
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
1h ago
READ MORE →
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
11h ago
READ MORE →
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
12h ago
READ MORE →
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
12h ago
READ MORE →
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
16h ago
READ MORE →
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
19h ago
READ MORE →
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
20h ago
READ MORE →
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
20h ago
READ MORE →
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
21h ago
READ MORE →