Transfer - International

Tetesi za soka Ulaya, Jumatatu March 11 2024

Joel JJ By Joel JJ
β€’
11 Mar 2024
Tetesi za soka Ulaya, Jumatatu March 11 2024

Machester United itafanya kila iwezalo kumsajili mshambuliaji wa Bayern Munich na Uingereza Harry Kane, 30, iwapo atapatikana msimu huu wa joto. (Give Me Sport)

Mmiliki mpya wa Manchester United Sir Jim Ratcliffe anatazamiwa kuidhinisha dau la zaidi ya pauni milioni 100 kwa kiungo wa kati wa Benfica Mreno Joao Neves, 19. (Mirror, via Mail)

Liverpool wamemchagua meneja wa Brighton Roberto de Zerbi, kocha wa Ujerumani Julian Nagelsmann na Ruben Amorim wa Sporting Lisbon kugombea nafasi ya Jurgen Klopp. (Football Insider)

Kiungo wa kati wa Ujerumani Joshua Kimmich, ambaye amekuwa akihusishwa na Manchester United, Manchester City na Liverpool, bado hajafanya mazungumzo ya kandarasi na Bayern Munich ikiwa imesalia chini ya miezi 18 katika mkataba wa sasa wa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 29. (90 min)

Arsenal wako tayari kumuuza beki wao Kieran Tierney msimu huu wa joto lakini The Gunners wanataka pauni milioni 20 kwa mlinzi huyo wa Scotland mwenye umri wa miaka 26. (Give Me Sport)

Chelsea bado hawajafanya maamuzi kuhusu mustakabali wa kiungo wa kati wa Uingereza Conor Gallagher, 24, licha ya Tottenham kumtaka. (Caught offside)

Chelsea huenda ikawauza wachezaji 15 katika dirisha la usajili la majira ya kiangazi. (Football.London)

Manchester United inanuia kuongeza mshahara wa kiungo wa kati wa Uingereza Kobbie Mainoo, 18, mara tatu chini ya mwaka mmoja baada ya kusaini mkataba mpya, ili kumbakisha klabuni hapo hadi 2030. (Sun)

AC Milan bado wanafanya mazungumzo na Arsenal kuhusu uhamisho wa beki wa Poland Jakub Kiwior, 24. (Fichajes, via Team Talk)

BBC

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
1h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
2h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
3h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
5h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
19h ago
READ MORE β†’