Simba - Local

Matola anaamini mbio za ubingwa ziko wazi

Joel JJ By Joel JJ
β€’
12 Mar 2024
Matola anaamini mbio za ubingwa ziko wazi

Kocha Msaidizi wa Simba, Selemani Matola, amesema mechi bado zipo nyingi ambazo zinaweza kuipatia Simba ubingwa wa Tanzania Bara, lakini amesisitiza ni lazima wachezaji waongeze umakini na kutumia vyema nafasi nyingi wanazotengeneza katika kila mechi

Matola amesema hawapaswi kukata tamaa kwa kuangalia matokeo ya timu nyingine kwa sababu ligi ni kama mbio ndefu, anayechanga karata zake vizuri mwishoni mwa kumalizika ndiyo mshindi na si yule anayeongoza kwa muda mrefu

"Siwezi kusema eti ubingwa basi kwa sababu kuna timu inafanya vizuri, sisi bado tupo kwenye mbio hizo na tuna imani tunaweza kuupata"

"Siku zote ligi ni kama mbio ndefu, mwanariadha anaweza kuongoza kwa muda mrefu, akawa mbele kilometa nyingi, lakini zikibaki mita kadhaa watu wanapindua kibao, hii ni raundi ya 20, lakini sisi Simba tumecheza mechi 17, hivyo michezo mingi imebaki , huwezi kututoa kwenye ubingwa," alisema Matola.

Matola pia amezungumzia changamoto ya ratiba ambayo inawanyima muda wa kufanya maboresho zaidi ya kimbinu kwa sababu ya kucheza kila baada ya siku mbili

"Ratiba ni changamoto pia, wakati mwingine tunakosa muda wa kufanya baadhi ya maandalizi kwa kuwa kila baada ya siku mbili tunacheza mechi"

"Tunaishia kufanya mazoezi ya 'recovery' kuwaandaa wachezaji na mechi inayofuata lakini yote kwa yote tutaendelea kupambana, timu inawachezaji bora na wengine wana uzoefu mkubwa naamini watatusaidia kufikia malengo yetu"

Leo saa 2:15 usiku Simba itashuka dimba la Azam Complex kumenyana na Singida FG ukiwa mchezo wa raundi ya 18 NBC PL

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
47m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
2h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
4h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’