Kocha Mkuu wa Yanga Miguel Gamondi amefichua mkakati wa kuiwinda Mamelodi Sundowns kimya-kimya akibainisha kuwa wanajiandaa kikamilifu kuhakikisha wanashinda mchezo wa mkondo wa kwanza robo fainali ligi ya mabingwa utakaopigwa Jumamosi, March 30
Inafahamika, Mamelodi walituma watu wao mapema kuja kuisoma Yanga jambo ambalo Gamondi na benchi lake la ufundi walilibaini na hivyo kubadili mbinu za maandalizi kuelekea mchezo huo
Yanga kwa sasa inafanya maandalizi yake katika uwanja wa Bandari na sio Avic Town ambako ndiko iliko kambi ya mabingwa hao wa Tanzania Bara
"Sisi hatujalala tupo kazini, tunafahamu kila kitu kuhusu Mamelodi Sundowns, tumeamua kwenda kupambana nao kimya kimya"
"Kila kitu kuhusu ufundi wao wakiwa ugenini tayari tunavyo muda mrefu tukiendelea kuvifanyia kazi. Bahati kubwa kwetu ni kwamba tuna benchi la ufundi ambalo mbali na kuijua Mamelodi pia tumefanikiwa kupata Kila taarifa zao ambazo zitatusaidia kutimiza mipango yetu ya kupata ushindi"
"Tunachokiomba tu ni wachezaji wetu kurejea wakiwa salama kwenye majukumu ya timu zao za Taifa, tumeacha wao waseme mitandaoni, hatujatoka mchezoni kama ambavyo watu wanavyoichukulia hii mechi, tunawaheshimi Mamelodi lakini dakika 90 za nyumbani tunapaswa kuonyesha ukubwa wetu," alisema Gamondi
Mkakati wa 'kuwapoteza maboya' Mamelodi ulianza tangu katika mchezo wa ligi kuu dhidi ya Geita Gold, Mamelodi watarajie kukutana na Yanga iliyokamili siku ya Jumamosi



