Kocha Mkuu wa Simba Abdelhak Benchikha amesema yeye na wachezaji wake hakuna jambo wanafikiria zaidi ya kupata ushindi dhidi ya Al Ahly na kutinga nusu fainali ya michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika
Kesho Ijumaa Simba itakuwa mwenyeji wa Al Ahly katika mchezo wa mkondo wa kwanza robo fainali CAF CL ambao utapigwa uwanja wa Benjamin Mkapa, saa 3 usiku
Akizungumza katika Mkutano na Wanahabari kuelekea mchezo huo, Benchikha amesema hakuna jambo lisilowezekana, wanayo nafasi ya kupata ushindi dhidi ya Al Ahly na kutinga nusu fainali
Benchikha amewataka mashabiki wa Simba kuwa na imani na timu yao, wajitokeze kwa wingi uwanja wa Benjamin Mkapa hapo kesho
"Nataka kuivusha Simba Robo fainali na kwenda Nusu fainali, hayo ni malengo yangu hadi wachezaji, nataka tuende mbele zaidi tofauti na ambapo Simba huwa inafikia"
"safari hii nataka kuivusha Simba na najua wachezaji wangu wapo tayari. Hakuna kitu kigumu katika mpira, sisi Simba tunaenda kupigana kwenye hatua hii kuanzia nyumbani hadi ugenini"
"Kikubwa mashabiki wetu kuwa na imani na sisi na kujitokeza kwa wingi uwanjani kuwaunga mkono wachezaji katika mchezo huu muhimu," alisema Benchikha



