Yanga - Local

Mzize apotezea kelele za mashabiki

Joel JJ By Joel JJ
β€’
12 Apr 2024
Mzize apotezea kelele za mashabiki

Mshambuliaji Clement Mzize, amesema hatasikiliza 'kelele' za mashabiki na badala yake ataendelea kufuata maelekezo anayopewa na kocha wake, Miguel Gamondi, ili kuisaidia timu Yanga kupata matokeo mazuri katika mechi zake

Juzi Mzize aliiongoza Yanga kutinga robo fainali ya kombe la Shirikisho la CRDB akifunga bao la pili katika ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Dodoma Jiji

Nyota huyo ambaye bado ni 'kinda', amesema anafurahi kuona Gamondi anampa nafasi ya kucheza na anamwamini hali inayomtengenezea kujiamini na kufanya vizuri

Mzize alisema licha ya kutofanya vizuri katika michezo miwili iliyopita jambo lililozalisha 'maneno' juu yake, aliongeza bado hatayapa nafasi anapokuwa uwanjani.

"Mara nyingi Kocha Miguel ananiambia natakiwa kufuata maelekezo yake anayonipa mazoezi na kuhamishia uwanjani, ananiamini na nisipaniki, nisitoke mchezoni kwa sababu ya kutofanya vizuri katika mechi mbili zilizopita"

"Nitajituma na kupambana kila ninapopata nafasi ya kucheza ili kuhakikisha ninafunga na kutafuta tuzo ya ufungaji bora wa michuano hiyo (Kombe la FA), sitasikiliza maneno ya nje," alisema Mzize

Mzize ndio kinara wa mabao katika michuano ya FA akifunga mabao matano

More Stories

Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
26m ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
1h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
2h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
3h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
3h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
16h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
16h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
17h ago
READ MORE β†’
Clement Mzize arejea rasmi kikosini baada ya miezi sita nje kwa majeraha
Clement Mzize arejea rasmi kikosini baada ya miezi sita nje kwa majeraha
22h ago
READ MORE β†’