Simba - Local

Ahmed Ali awatuliza mashabiki wa Simba baada ya kipigo

Joel JJ By Joel JJ
22 Apr 2024
Ahmed Ali awatuliza mashabiki wa Simba baada ya kipigo

Licha ya maumivu makali ambayo Wanasimba wanapitia kutokana na mwenendo wa timu yao, Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Wekundu hao wa Msimbazi Ahmed Ally amewataka kuendelea kuwa uvumilivu kwani nyakati za furaha zinakuja

Juzi Simba ilipoteza mchezo wa pili msimu huu dhidi ya watani zao Yanga kwa kufungwa mabao 2-1 katika mchezo uliopigwa uwanja wa Benjamin Mkapa

Ulikuwa mchezo wa tano mfululizo Simba inakosa ushindi katika michuano yote

Kupitia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii, Ahmed amewapa Wanasimba ujumbe huu;

"Dhahabu hupitishwa kwenye moto mkali ili ipate thamani na iwe bora

Licha ya kuwa huteseka inapopita kwenye moto huo lakini mwishoe hubaki safi, bora na thamani yake huongezeka maradufu

Wana Simba tuvumilie kupita kwenye moto huu mkali ili tuwe bora na hadhi yetu irejee

Najua maumivu ni makubwa kwa kua moto mkali lakini hatuna budi kuvumilia kwani ndio njia pekee ya kurudi kwenye thamani yetu"

Kikosi cha Simba kinaelekea Zanzibar kushiriki Muungano Cup ambapo Jumatano itashuka uwanja wa New Amaan Complex kuikabili KVZ katika mchezo wa nusu fainali

More Stories

SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa  Yanga SC “Your next: Yanga”
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa Yanga SC “Your next: Yanga”
1m ago
READ MORE →
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
1h ago
READ MORE →
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
11h ago
READ MORE →
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
12h ago
READ MORE →
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
12h ago
READ MORE →
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
16h ago
READ MORE →
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
19h ago
READ MORE →
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
20h ago
READ MORE →
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
20h ago
READ MORE →
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
21h ago
READ MORE →