Yanga - Simba - Azam - Local

Serikali yaja na mkakati Afcon 2027

Joel JJ By Joel JJ
β€’
30 Apr 2024
Serikali yaja na mkakati Afcon 2027

Serikali ina mpango wa kuunda timu tatu imara za soka za Taifa kulingana na umri ambazo zitashiriki mashindano ya Afcon 2027 na mengine ambayo nchi itashiriki

Naibu Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Hamis Mwinjuma amesema hayo leo Jumatatu Aprili 30, 2024 alipojibu maswali ya nyongeza ya Mbunge wa Jimbo la Magomeni, Mwanakhamis Kassim Said (CCM)

Mbunge huyo amehoji Serikali ina mkakati gani wa kuandaa timu ya Taifa ili ishindane kwenye michuano ya Afcon. Pia amehoji ni kwa jinsi gani wasanii watashirikishwa kwenye fainali za Afcon 2027

Naibu Waziri, Mwinjuma amesema Serikali imeandaa mkakati wa kuandaa timu si tu kwa ajili ya Afcon 2027, bali kwa mashindano mengine ambayo Tanzania itashiriki na zitagharamiwa na Serikali kwa asilimia 100

Amesema moja ya mkakati ni kutengeneza timu tatu za Taifa zitakazopishana umri ya kwanza itakuwa ni ya vijana chini ya miaka 17, itakayotokana na wanafunzi wa michezo ya Umiseta ya kila mwaka

"Tukishawapata wachezaji hawa tutawaweka kwenye shule moja ambayo tumeshaiteua na watasimamiwa na walimu magwiji. Itapata mechi za mazoezi ya kutosha za ndani na nje. Kila mwaka wachezaji hao tutakuwa tunawapeleka kwenye akademi zenye mafanikio nje ya nchi ili kuendeleza vipaji tayari kulitumikia Taifa," amesema

Mwinjuma amesema timu ya pili, itakuwa inayoundwa na vijana wenye umri wa chini ya miaka 23, ambao wanacheza ligi mbalimbali ndani na nje ya nchi na watakuwa wakikutana wakati wakiwa kwenye mapumziko ya timu zao

Mwinjuma amesema Tanzania kwa kushirikiana na nchi za Kenya na Uganda itakuwa mwenyeji wa mashindano ya Afcon 2027

"Ili kuhakikisha timu ya Taifa inafanya vizuri katika mashindano hayo, Serikali imeweka mikakati mbalimbali ikiwemo ujenzi wa viwanja vya mpira katika majiji ya Dodoma na Arusha," amesema

Amesema pia utafanyika ukarabati wa Viwanja vya Benjamin Mkapa na Uhuru, na kuwatafuta na kuwaleta nchini wachezaji wenye asili ya Tanzania wanaoishi na kucheza nje ya nchi ili kuchezea timu ya Taifa.

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
45m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
2h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
4h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’