Yanga - Local

Yanga yatangaza sherehe za ubingwa Ligi Kuu

Joel JJ By Joel JJ
β€’
20 May 2024
Yanga yatangaza sherehe za ubingwa Ligi Kuu

Meneja wa Habari na Mawasiliano klabu ya Yanga Ali Kamwe amesema kikosi kinarejea jioni ya leo kutokea Arusha baada ya ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Ihefu Fc jana na kutinga fainali ya kombe la Shirikisho la CRDB

Kamwe amesema kikosi kitafanya mazoezi Arusha.  Jumanne asubuhi Yanga itaelekea Dodoma kuikabili Dodoma Jiji May 22

Katika mchezo dhidi ya Dodoma Jiji siku ya Jumatano, Yanga itapata heshima 'guard of honor' kwa kutwaa ubingwa mapema

Hii itakuwa mechi maalum ya kushukuru benchi la ufundi kwa kuhakikisha Yanga imetwaa ubingwa wa 30. Itakuwa 'Gamond Day'

Katika mchezo huo itakapofika dakika ya 30, mashabiki wote watasimama kumpigia makofi Gamondi na benchi lake la ufundi kwa kazi nzuri ya kuipa Yanga ubingwa wa 30

Wale watakaoweza kutengeneza picha ya Gamondi, watasimama nayo katika dakika ya 30

May 23 Yanga imealikwa na Wizara ya Sanaa, Utamaduni na Michezo chini ya Waziri Dk Damas Ndumbaro kuhudhuria Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Kikosi cha Yanga kitarejea jijini Dar es Salaam jioni ya May 23 kwa ajili ya maandalizi ya mchezo dhidi ya Tabora United

May 25 Yanga itakabidhiwa ubingwa katika mchezo dhidi ya Tabora United utakaopigwa uwanja wa Benjamin Mkapa

Yanga imetangaza May 25 ni siku ya kibingwa kwa mashabiki wa Yanga kuelekea uwanja wa Benjamin Mkapa kwenda kukabidhiwa taji la ligi kuu ambalo wataondoka nalo moja kwa moja

Mageti ya Benjamin Mkapa yatafunguliwa saa 5 asubuhi tayari kwa mashabiki kuingia uwanjani. Kutakuwa na burudani za muziki kutoka kwa wasanii wakubwa wa ndani na nje ya nchi

Lakini pia, kutakuwa na suprise kubwa itashuhudiwa saa 5 asubuhi katika jiji la Dar es salaam

Viingilio VIP A - SOLD OUT, VIP B - Tsh 10,000/-, VIP C - Tsh 5,000/- na Mzunguuko - Tsh 1,000/-

Baada ya mchezo kumalizika, sherehe za ubingwa ndio zinaanza rasmi, kutakuwa na mkesha wa ubingwa!

May 26 kombe litaondoka dimba la Benjamin Mkapa kuelekea Jangwani yalipo Makao Makuu ya Yanga. Hivyo Parade la Ubingwa mwaka huu litaanzia Benjamin Mkapa kuelekea Jangwani

Kabla ya Parade saa 2 asubuhi Wananchi wakakunywa supu ya ubingwa pale kwa Mkapa ambapo mpaka sasa tayari ng'ombe 11 wameandaliwa

Baada ya supu parade la ubingwa kuelekea Jangwani itaanza rasmi kupitia barabara maalum zitakazotangazwa

More Stories

Klopp amchagua ter stegen, kipa namba moja ujerumani
Klopp amchagua ter stegen, kipa namba moja ujerumani
1m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
29m ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
1h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
2h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
3h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
3h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
16h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’