Transfer - International

Tetesi za usajili Ulaya, Jumanne May 21 2024

Joel JJ By Joel JJ
β€’
21 May 2024
Tetesi za usajili Ulaya, Jumanne May 21 2024

Meneja wa Burnley Vincent Kompany, 38, ni miongoni mwa watu wanaopigiwa upatu kuchukua nafasi ya Thomas Tuchel huko Bayern Munich . (Fabrizio Romano)

Aston Villa wanakaribia kufikia makubaliano ya kumnunua tena mchezaji wa Luton Town na kiungo wa kati wa zamani wa Uingereza Ross Barkley kwa mkataba wa kudumu, miaka minne baada ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 30 kujiunga kwa mkopo kutoka Chelsea(Guardian)

Arsenal wanataka kusajili mshambuliaji kabla ya ziara yao ya kujiandaa na msimu mpya, huku nyota wa Newcastle United na Uswidi Alexander Isak, 24, na mshambuliaji wa Ajax na Uholanzi, Brian Brobbey, wakiongoza orodha hiyo.(Independent)

Chelsea na Manchester United zote zimewasiliana na mkufunzi wa Ipswich Town Kieran McKenna, huku raia huyo wa Ireland Kaskazini akiwa katika harakati za kuchukua nafasi ya Mauricio Pochettino au Erik ten Hag. (Manchester Evening News)

Wolves itadai kiasi cha kuvunja rekodi ya klabu cha pauni milioni 60 kwa winga wa Ureno mwenye umri wa miaka 24 Pedro Neto, ambaye analengwa na Manchester City na Newcastle msimu wa joto(Telegraph )

Aston Villa wako tayari kusikiliza ofa kwa mlinzi wa Brazil Diego Carlos, 31, huku wakitarajia kufuata sheria za faida na uendelevu(Telegraph)

Mkufunzi wa Villa Unai Emery anataka kumsajili beki wa Barcelona na Uruguay Ronald Araujo, 25. (Sport kwa Kihispania)

Stoke wameonyesha nia ya kutaka kumsajili beki wa Uingereza Conor Coady, 31, kutoka Leicester(Teamtalk)

Leicester wanajiandaa kushindana na vilabu vya Ufaransa Lyon na Brest kumnunua fowadi wa Burkina Faso Mohamed Konate, 26, ambaye mkataba wake na klabu ya Urusi Akhmat Grozny unamalizika msimu huu. (Football Insider)

Meneja wa Tottenham Ange Postecoglou ameiomba klabu hiyo takriban wachezaji watatu wapya msimu huu wa joto. (ESPN) Manchester United wanavutiwa na mlinzi wa Everton Muingereza Jarrad Branthwaite, 21, na The Toffees wanaweza kumnunua beki wa kati wa Galatasaray na Colombia Davinson Sanchez, 27, kuziba nafasi yake.(Caught Offside)

Tottenham wako tayari kumuuza mlinzi wa Brazil Emerson Royal, 25, huku Juventus , AC Milan na Bayern Munich zikiwa na hamu ya kumnunua (Givemesport)

Newcastle wanaweza kumnunua Lloyd Kelly, 25, huku beki huyo wa Uingereza akitarajiwa kuondoka Bournemouth kama mchezaji huru. (Fabrizio Romano)

Chelsea itadai ada ya pauni milioni 25 kwa mlinzi wa Uingereza Trevoh Chalobah, 24, ambaye anatarajiwa kuvutia vilabu kadhaa (Telegraph)

Rais wa Corinthians Augusto Melo atasafiri hadi Uingereza wiki ijayo kuzungumza na vilabu kuhusu uwezekano wa kuuzwa kwa mshambuliaji wa Brazil Wesley mwenye umri wa miaka 19. (Globo Esporte - kwa Kireno)

BBC

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
1h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
2h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
3h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
5h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
19h ago
READ MORE β†’