Fainali ya kombe la Shirikisho la Bank ya CRDB sasa itachezwa katika uwanja wa New Amaan Complex, Zanzibar badala ya Babati mkoani Manyara
Taarifa iliyotolewa na TFF mapema leo, imebainisha kuwa sababu ya mabadiliko ya uwanja imetokana na kutokamilika kwa baadhi ya miundombinu muhimu huko Babati pamoja na sababu za kiusalama
Mchezo huo wa fainali kati ya Azam Fc dhidi ya Yanga utapigwa Juni 02, saa 2:15 usiku