KMC yagomea mechi dhidi ya Simba kupigwa Arusha

Joel JJ By Joel JJ β€’ 23rd May 2024


KMC yagomea mechi dhidi ya Simba kupigwa Arusha

Klabu ya KMC imedai kuwa haitambui mabadiliko ya uwanja wa mchezo wa ligi kuu dhidi ya Simba ambao utapigwa uwanja wa Sheikh Amri Abeid Jumamosi May 25 2024

Msemaji wa klabu hiyo Khalid Chukuchuku amesema kulingana na kanuni za ligi, taarifa ya mabadiliko ya uwanja ilipaswa kutolewa siku saba kabla ya mchezo husika

Chukuchuku amesema KMC ilitaarifiwa Jumamosi iliyopita kuwa mchezo kati yake na Simba utapigwa uwanja wa Meja Jen. Isamuhyo hivyo hawatambui mabadiliko hayo kwa kuwa yako nje ya muda uliotajwa kikanuni

"Ukisoma kanuni zinakwambia taarifa ya mabadiliko ya uwanja inatakiwa itolewe siku 7 kabla ya mchezo, Jumamosi iliyopita tulipewa taarifa mchezo utachezwa Katika Uwanja wa Meja Jenerali isamuhyo"

"Zimebakia siku tatu kabla ya mchezo tunaona taarifa kuwa kuna mabadiliko ya uwanja kanuni zimevunjwa sisi tunajiandaa kucheza mchezo wetu katika uwanja wa Isamuhyo"

"Ukisema kwamba Dar es salaam siku hiyo viwanja vitakuwa vimejaa ni uongo siku ya Jumamosi uwanja wa Isamuhyo utakuwa hautumiki kwa sababu JKT Tanzania watakuwa Tanga dhidi ya Coastal Union, Lazima tuzingatie kanuni zilizowekwa, " alisema Khalid


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.