Simba inatajwa kukamilisha usajili wa kiungo mshambuliaji wa Asec Mimosas Serge Pokou
Simba ilifungua mazungumzo na kiungo huyo tangu mwezi April na kilichokuwa kinasubiriwa ni msimu kufika tamati ili nyota huyo ajiunge na Simba akiwa mchezaji huru
Pokou mwenye umri wa miaka 23 alikuwa na mkataba wa mwaka mmoja na Asec ambao umemalizika baada ya msimu kwisha
Pokou ataungana na Aubin Kramo kuitumikia Simba msimu ujao wote wakitokea klabu ya Asec Mimosas
Pokou alikuwa kiungo tegemeo katika kikosi cha Asec akifunga mabao matatu na asisti moja katika Ligi ya Mabingwa Afrika ambapo aliisaidia Asec kucheza hatua ya robo fainali wakitolewa na Esperance kwa mikwaju ya penati
Nyota huyo pia ameifungia Asec mabao 8 katika ligi kuu ya Ivory Coast ambapo Asec walimaliza msimu wakiwa nafasi ya nne



