Kamwe atamba kuhusu usajili Yanga

Joel JJ By Joel JJ β€’ 7th June 2024


Kamwe atamba kuhusu usajili Yanga

Meneja wa Habari na Mawasiliano klabu ya Yanga Ali Kamwe ametamba kuwa katika usajili wa dirisha hili watashusha wachezaji bora na wenye majina makubwa

Baada ya msimu kuhitimishwa shauku ya kila Mwananchi ni kufahamu mikakati ya kuelekea msimu ujao wengi wakisubiri kwa hamu taarifa za usajili

Msemaji huyo wa Yanga amesema kila kitu kitaenda kama kilivyopangwa akiwahakikishia Wanachama na Mashabiki wa Yanga kuwa furaha yao itaendelea hata pale dirisha la usajili litakapofunguliwa

"Uongozi unasubiri ripoti ya benchi la ufundi kuhusu wachezaji ambao watahitaji kuendelea nao pamoja na maboresho kuelekea msimu ujao"

"Niwaambie tu, kama alivyosema Rais wa Yanga Injinia Hersi Said, msimu ujao tumeweka malengo makubwa hasa kufanya vizuri katika michuano ya ligi ya mabingwa"

"Hivyo wachezaji wote ambao benchi la ufundi litapendekeza tuendelee nao msimu ujao watabaki. Tukiwa timu yenye malengo ya kuliteka soka la Afrika, lazima tuhakikishe wachezaji wetu bora wanabaki"

"Lakini pia tutafanya maboresho ambayo yataendana na mahitaji ya malengo tuliyoweka msimu ujao. Katika usajili uliopita tulileta wachezaji wenye 'quality' lakini hawakuwa na majina makubwa. Safari hii tunashusha wachezaji wenye quality lakini pia wana majina makubwa," alitamba Kamwe

Aidha Kamwe amesema ile ahadi ya usajili wa mchezaji ambaye bango lake litawekwa mkabala na yalipo Makao Makuu ya klabu moja hapo Kariakoo, itatekelezwa


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.