Uongozi wa Klabu ya Singida Black Stars umeikamilisha usajili wa Kocha, Patrick Aussems raia wa Ubeligiji kuwa Kocha Mkuu wa timu huyo kuanzia msimu mpya wa 2024/25 kwa kandarasi ya awali ya msimu mmoja mpaka tarehe 30 June 2025 kama Kocha Mkuu
Patrick Aussems mwenye umri wa miaka 59 ni Kocha mwenye leseni ya UEFA PRO na uzoefu wa kufundisha vilabu vikubwa barani Afrika, Ulaya na Asia, zikiwemo timu za Al Hilal Omdurman (Sudan), Simba SC (Tanzania), AFC Leaopards (Kenya), Shenzhen Ruby (China), ETG (Evian Thonon Gaillard) FC na Angers SCO FC – France
Aussems anakubwa hapa Tanzania kwa mafanikio aliyoipa klabu ya Simba 2018/19 na 2019/20 akitwaa taji la ligi kuu na kucheza robo fainali ya ligi ya mabingwa barani Afrika



