Kupitia Mkutano Mkuu wa Wanachama wa Yanga uliofanyika ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano, Julius Nyerere, Rais wa Yanga Injinia Hersi Said amewahakikishia Wanachama na Mashabiki wa timu hiyo kuwa Kocha Miguel Gamondi ataendelea kuitumikia Yanga kwa msimu mwingine
Gamondi ndio surprise waliokuwa wameahidiwa Wanachama wa Yanga kwani aliibuka katika Mkutano huo na kuthibitisha bado yupo
"Nafuraha kubwa kuwa hapa. Kipekee namshukuru Rais Injinia Hersi Said, wenzangu katika benchi la ufundi na wachezaji wote"
"Nimefanya kazi katika nchi zaidi ya 40 lakini nikiri kwamba najisikia furaha zaidi hapa. Nawashuru Wananchi kwa kuniunga mkono katika mwaka huu ambao tumekuwa sote"
"Niwathibitishie nitaendelea kuwa hapa kwa msimu mwingine. Naamini kwa pamoja tutafanya makubwa zaidi ya msimu uliopita," alisema Gamondi
Rais wa Yanga Injinia Hersi Said amemtaka kocha huyo kuhakikisha wanatetea mataji waliyoshinda msimu uliopita yaani ligi kuu na kombe la FA lakini zaidi kufanya vizuri zaidi katika michuano ya ligi ya mabingwa