Chama atambulishwa Yanga

Joel JJ By Joel JJ β€’ 1st July 2024


Chama atambulishwa Yanga

Aliyekuwa kiungo mshambuliaji wa Simba Clatous Chama, amejiunga na Yanga, mabingwa hao wa Tanzania Bara wakimtambulisha mapema leo

Imeelezwa kuwa Chama amesaini mkataba wa mwaka mmoja ambao una kipengele cha kuongeza mwaka mwingine mwishoni mwa msimu

Tetesi kuhusu usajili wa Chama zilitawala katika dirisha hili la usajili lakini hatimaye Mwamba huyo wa Lusaka amemaliza misimu yake 6 ya kuitumikia Simba

Kulikuwa na matumaini kwa mashabiki wa Simba walioamini nyota huyo angeweza kuongeza mkataba katika klabu yao

Lakini taarifa ya Yanga mapema Jumatatu, imeondoa matumaini hayo, msimu ujao Chama kwa mara ya kwanza hapa Tanzania ataitumikia timu nyingine na sio Simba


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.