Aliyekuwa kiungo mshambuliaji wa Simba Clatous Chama, amejiunga na Yanga, mabingwa hao wa Tanzania Bara wakimtambulisha mapema leo
Imeelezwa kuwa Chama amesaini mkataba wa mwaka mmoja ambao una kipengele cha kuongeza mwaka mwingine mwishoni mwa msimu
Tetesi kuhusu usajili wa Chama zilitawala katika dirisha hili la usajili lakini hatimaye Mwamba huyo wa Lusaka amemaliza misimu yake 6 ya kuitumikia Simba
Kulikuwa na matumaini kwa mashabiki wa Simba walioamini nyota huyo angeweza kuongeza mkataba katika klabu yao
Lakini taarifa ya Yanga mapema Jumatatu, imeondoa matumaini hayo, msimu ujao Chama kwa mara ya kwanza hapa Tanzania ataitumikia timu nyingine na sio Simba



