Yanga - Local

Yanga hiyooo Afrika Kusini

Joel JJ By Joel JJ
β€’
16 Jul 2024
Yanga hiyooo Afrika Kusini

Alhamisi ya wiki hii Yanga inatarajiwa kusafiri Afrika Kusini kushiriki michuano maalum Mpumalanga Premier’s International Cup

Michuano hiyo imedhaminiwa na Shirika la utangazaji la Afrika Kusini (SABC) kwa kushirikiana na TS Galaxy Foundation

Ni michuano maalum ya pre-season ambayo pamoja na Yanga, timu nyingine zitakazoshiriki ni TS Galaxy Fc, Mbabane Swallows Fc na Augsburg inayoshiriki Ligi Kuu ya Ujerumani (Bundesliga)

Augsburg ilianzishwa mwaka 1907, ni klabu kubwa zaidi ya soka katika Swabian Bavaria yenye wanachama 25,000, ilipanda daraja Bundesliga kwa mara ya kwanza mwaka 2011, ambako imebaki tangu wakati huo. Katika msimu wa 2015/16, ilicheza Ligi ya Europa kwa mara ya kwanza

Augsburg itachuana na Yanga katika mchezo wa ufunguzi wa michuano hiyo utakaopigwa Jumamosi, Julai 20, Mbombela Stadium moja ya viwanja vilivyotumika katika michuano ya kombe la Dunia mwaka 2010

SABC watarusha mechi hiyo mbashara pamoja na mechi nyingine zitakazofuata

Baada ya mchezo huo, Wananchi wataendelea kusalia Afrika Kusini kujiandaa na mchezo wa Toyota Cup dhidi ya Kaizer Chiefs utakaopigwa Jumapili, Julai 28

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
44m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
2h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
4h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’