Rais wa klabu ya Yanga Injinia Hersi Said ambaye pia ni Mwenyekiti wa Umoja wa klabu barani Afrika (ACA) leo ameibuka Avic Town kushuhudia mazoezi ya kikosi cha Yanga ikiwa ni siku ya sita ya pre-season
Hersi alikuwa Afrika Kusini kwa wiki kadhaa akitekeleza majukumu yake kama Rais wa Yanga na Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la soka barani Afrika (CAF)
Hersi ameibuka wakati zikiendelea kusambaa taarifa kuwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Jijini Dar es salaam, imeamuru Uongozi wa Yanga ukiongozwa na Rais wa Yanga Injinia Hersi Saidi na wenzake, kuachia ngazi na kuondoka kwenye klabu hiyo kwa kuwa Katiba ya Yanga haitambui uwepo wao.



