Yanga - Local

Ausburg yaiongezea mzuka Yanga

Joel JJ By Joel JJ
β€’
21 Jul 2024
Ausburg yaiongezea mzuka Yanga

Licha ya timu yake kupoteza mchezo wa ufunguzi michuano ya Mpumalanga Premier's International Cup dhidi ya Augsburg, Kocha Mkuu wa Yanga Miguel Gamondi amesema ameridhishwa na kiwango klichoonyeshwa na vijana wake

Yanga ilifungwa mabao 2-1 katika mchezo ambao ilionyesha ubora mkubwa katika kipindi cha pili

Gamondi amesema ilikuwa heshima kubwa kwa Yanga kucheza na Augsburg inayoshiriki ligi kuu ya Ujerumani na anaamini kile walichokionyesha katika mchezo huo kimemfurahisha kila mpenda soka barani Afrika

"Hatukucheza vizuri sana kwenye kipindi cha kwanza kulikuwa makosa ya hapa na pale lakini hii ni kawaida hasa ukizingatia tulifanya mazoezi kwa wiki moja tu kabla ya mchezo huu ambao pia ni wa kwanza kwetu katika pre-season"

"Lakini pia tusisahau tumecheza dhidi ya Augsburg, timu ya ligi kuu ya Ujerumani (Bundesliga) hivyo isingekuwa rahisi kwa wachezaji wetu"

"Kipindi cha pili tulikuwa bora zaidi, tulifunga bao na pia tulikuwa na nafasi dakika za mwisho tungeweza kusawazisha"

"Matokeo hayakuwa muhimu sana kwetu katika mchezo huu. Nimefurahishwa na vile wachezaji wangu walivyopambana na kufanya kile tulichohitaji kutoka kwao," alisema Gamondi

Yanga itacheza mechi nyingine mbili hapo Afrika Kusini kabla ya kurejea Tanzania tayari kwa wiki ya Mwananchi

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
1h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
2h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
3h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
5h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
19h ago
READ MORE β†’