Kocha Simba afurahia ushindi wa kwanza Misri

Joel JJ By Joel JJ β€’ 23rd July 2024


Kocha Simba afurahia ushindi wa kwanza Misri

Baada ya ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya El Qanah katika mchezo wa kwanza wa kirafiki ambao Simba ilicheza jana Misri, Kocha Mkuu wa Simba Fadlu Davies ameeleza kuridhishwa kiwango kilichoonyeshwa na wachezaji wake katika mchezo huo

Fadlu amesema kile alichokifanyia kazi katika kipindi cha wiki mbili za pre-season huko Misri kimeanza kuonekana lakini huo ni mwanzo tu

"Nafurahi tumeweza kushinda mechi kwa mabao 3-0 lakini muhimu wachezaji wamecheza vizuri, baada ya wiki mbili za mazoezi, hii ni hatua nzuri kwetu"

"Hii ni mechi maalum ya kimkakati zaidi, tulianza vyema na kufunga mabao mawili katika kipind cha kwanza kama tusingefanya mabadiliko ya wachezaji tulikuwa na nafasi ya kufunga hata mabao matano"

"Ilikuwa mechi ambayo tulilenga kumpa nafasi kila mchezaji ili tuone ni kwa namna gani tumefanikiwa katika maandalizi yetu. Kila mchezaji alipata angalau dakika 30 za kucheza ni wachezaji wawili tu (Awesu na Onana) ambao walichelewa kuungana nasi hapa Misri hivyo walicheza kwa dakika 20"

"Baadhi ya wachezaji tuliwapa muda zaidi (dakika 60) kwa kuzingatia utimamu na utayari wao baada ya muda huu mfupi wa mazoezi"

"Lakini nisema bado tuna kazi ya kufanya, kwa wastani tulihitaji angalau wiki sita za maandalizi. Tuna timu mpya wachezaji wengi hapa ni wageni, tunahitaji kuwajenga kimbinu pamoja na kupata mechi zaidi za kirafiki"

"Mpaka kufikia Simba Day tutakuwa tumepata angalau wiki nne, bila shaka tutakuwa katika hatua nzuri zaidi na baada ya muda mfupi tutafikia malengo na matarajio yetu ya kuwa na timu bora na ya ushindani," alisema Fadlu


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.