Miamba ya soka la England klabu ya Manchester City inapanga kumfanya kiungo wa klabu ya Bayern Munich na timu ya taifa ya Ujerumani Jamal Musiala, 21, kuwa mrithi wa kiungo mchezeshaji wao Kevin de Bruyne, 33. (CaughtOffside)
Barcelona wamefikia makubaliano ya kumsajili winga wa klabu ya Athletic Bilbao na timu ya taifa ya Uhispania Nico Williams, 22, kwa mkataba wa miaka mitano, ambao pia utakuwa na kipengele cha nyongeza ya mwaka mmoja. (Nicolo Schira)
Tottenham ipo mbele ya Liverpool na Arsenal katika kinyang’anyiro cha kumsajili winga wa klabu ya Juventus na timu ya taifa ya Italia Federico Chiesa, 26. (Football Transfers)
Klabu ya Arsenal inataka kulipwa dau la walau euro milioni 50 (pauni 42m) ili kumuuza mshambuliaji wao raia wa Uingereza Eddie Nketiah, 25, ambaye mpaka sasa ameivutia klabu ya Ufaransa ya Marseille. (La Provence - in French)
Newcastle United wana imani kuwa winga wao Anthony Gordon atasalia kwenye klabu hiyo licha ya kufuatiliwa na Liverpool. (Team Talk)
West Ham wanajipanga kuongeza dau ili kumnasa mshambuliaji Jhon Duran, 20, kutoka Colombia ambaye klabu yake ya sasa Aston Villa inataka pauni milioni 40 ili kumuachia. (Standard)
Manchester United wamerejea katika mbio za kutaka kumsajili beki wa Bayern Munich na timu ya taifa ya Morocco Noussair Mazraoui, 26, baada ya mipango yake ya kuhamia West Ham kushindikana. (Sky Germany)
Mazraoui anatazamiwa kutaka kuhakikishiwa kuwa atapata muda wa kutosha wa kucheza kabla ya kukubali kujiunga na United. (Manchester Evening News)
Tottenham wapo kwenye mazungumzo na klabu ya Girona ili kuwauzia mshambuliaji wao raia wa Uhispania Bryan Gil, 23, ambaye tayari ameshaafikiana na Girona kuhusu maslahi yake binafsi. (Fabrizio Romano)
Manchester United wamefanya mazungumzo kuhusu uwezekano wa kubadilishana beki wao Aaron Wan-Bissaka, 26, na Denzel Dumfries, 28, kutoka Inter Milan. (Telegraph - subscription required)
Chelsea wanajiandaa kuwaruhusu wachezaji 12 kuondoka katika klabu hiyo kwenye dirisha hili la usajili baada ya mkataba wa beki wao raia wa Ufaransa Malang Sarr, 25, kuvunjwa ili kumuwezesha kujiunga na klabu ya RC Lens. (Sun)
Los Angeles FC wamepiga hatua katika mazungumzo yao kutaka kumsajili mshambuliaji wa klabu ya Atletico Madrid na timu ya taifa ya Ufaransa Antoine Griezmann, 33. (L'Equipe - in French)
Klabu hiyo inayocheza ligi ya Marekani (MLS) pia wapo karibu kumsajili kwa mkopo kiungo raia wa Uingereza Lewis O'Brien, 25, kutoka katika klabu ya Nottingham Forest. (Football Insider)
BBC



