Yanga yaichapa Kaizer Chiefs 4-0, yabeba Toyota Cup

Joel JJ By Joel JJ β€’ 28th July 2024


Yanga yaichapa Kaizer Chiefs 4-0, yabeba Toyota Cup

Yanga imebeba Toyota Cup ugenini ikiifumua Kaizer Chiefs mabao 4-0 katika mchezo uliopigwa uwanja wa Toyota Bloemfontein huko Afrika Kusini

Unaweza kusema ilikuwa mechi ya Yanga kudhihirisha umwamba mbele ya kocha wake wa zamani Nasreddine Nabi ambaye vijana wake walikuwa na wakati mgumu

Alikuwa ni Prince Dube aliyefungua kalamu ya mabao akitumia makosa ya safu ya ulinzi ya Chiefs kabla ya Aziz Ki kuongeza la pili akipokea pasi ya Duke Abuya

Yanga ilikwenda mapumziko ikiwa mbele kwa mabao 2-0 na ikarejea kipindi cha pili kuongeza mengine mawili kupitia kwa Aziz Ki na Clement Mzize

Aziz Ki alichaguliwa kuwa nyota wa mchezo huo ulioshuhudiwa na mashabiki takribani 46,000

Hii ilikuwa mechi inayohitimisha pre-season ya Yanga Afrika Kusini ambapo sasa Wananchi wanarejea nchini kwa ajili ya maandalizi ya mwisho ya wiki ya Mwananchi


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.