Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB), imemtangaza Ahmed Aragija kutoka Manyara kuwa mwamuzi wa kati wa mchezo wa Ngao ya Jamii utakaozikutanisha Azam FC na Coastal Union utakaopigwa, kesho, Alhamisi
Mchezo huo wa Ngao ya Jamii unatarajiwa kuchezwa kwenye Uwanja wa New Amaan, Zanzibar kuanzia saa 10:00 jioni huku Coastal Union ikiwa mwenyeji
Katika mchezo huo, Janeth Balama kutoka Iringa na Ally Ramadhani wa Zanzibar watakuwa waamuzi wasaidizi wakati Nasri Siyah kutoka Zanzibar pamoja na Victor Mwandike kutoka Mtwara ndio watakuwa waamuzi wa akiba
Agosti 8, 2024 ni ufunguzi wa msimu wa soka wa 2024-2025 nchini ambapo zinachezwa mechi za Ngao ya Jamii kuanzia hatua ya nusu fainali, kisha mshindi wa tatu ikifuatiwa na fainali



