Arajiga apewa Azam Fc v Coastal Union, Ngao ya Jamii

Joel JJ By Joel JJ β€’ 7th August 2024


Arajiga apewa Azam Fc v Coastal Union, Ngao ya Jamii

Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB), imemtangaza Ahmed Aragija kutoka Manyara kuwa mwamuzi wa kati wa mchezo wa Ngao ya Jamii utakaozikutanisha Azam FC na Coastal Union utakaopigwa, kesho, Alhamisi

Mchezo huo wa Ngao ya Jamii unatarajiwa kuchezwa kwenye Uwanja wa New Amaan, Zanzibar kuanzia saa 10:00 jioni huku Coastal Union ikiwa mwenyeji

Katika mchezo huo, Janeth Balama kutoka Iringa na Ally Ramadhani wa Zanzibar watakuwa waamuzi wasaidizi wakati Nasri Siyah kutoka Zanzibar pamoja na Victor Mwandike kutoka Mtwara ndio watakuwa waamuzi wa akiba

Agosti 8, 2024 ni ufunguzi wa msimu wa soka wa 2024-2025 nchini ambapo zinachezwa mechi za Ngao ya Jamii kuanzia hatua ya nusu fainali, kisha mshindi wa tatu ikifuatiwa na fainali


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.