Simba - Tabora - Local

Simba yatamba baada ya kuifumua Tabora United 3-0

Joel JJ By Joel JJ
β€’
19 Aug 2024
Simba yatamba baada ya kuifumua Tabora United 3-0

Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba Ahmed Ali amesema ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Tabora United katika mchezo wa kwanza ligi kuu ya NBC, ni ishara ya dhamira ya Simba kuwania taji la ligi kuu

Ahmed ametamba kuwa mkakati wa Simba ni kuhakikisha wanaendelea kubaki kileleni mwa msimamo wa ligi kwa kushinda kila mechi inayokuja mbele yao

Hata hivyo Ahmed amewataka mashabiki wa Simba kuwavumilia baadhi ya wachezaji wapya ambao wameanza taratibu majukumu yao na Simba

Ahmed amebainisha kuwa ni jambo la kawaida kwa mchezaji anapotoka timu moja kwenda nyingine wakati mwingine huhitaji muda kuzoea

"Pamoja na kushinda dhidi ya Tabora United lakini ukweli ni kuwa tunahitaji kuwapa muda zaidi wachezaji wetu waendelee kutafuta ubora wao"

"Tumesajili wachezaji bora sana ambao wamefanya makubwa walikotoka Katika hao wapo walioanzia juu moja kwa moja na wengine wameanzia chini, iko hivyo duniani kote hasa mchezaji anapotoka timu ndogo kwenda kubwa au kutoka ligi ndogo kwenda kubwa au anapoenda kwenye timu yenye presha kubwa kama yetu"

"Ni jukumu letu kuwavumilia, kuwatia moyo, kusimama nao nyakati zote ili warejeshe kujiamini na kuupata ubora wao"

"Aina ya wachezaji tuliokua nao nusu yao wakiupata ubora wao basi mwaka huu utakua Msimu mzuri kwetu INSHA ALLAH," aliandika Ahmed katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
47m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
2h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
4h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’