Shirikisho la mpira wa miguu Duniani (FIFA) limeitaka klabu ya Yanga kulipa Benchem United ya Ghana kiasi cha dola 80,000 (sawa na Sh 217 milioni) kutokana na usajili wa winga Augustine Okrah
Hukumu hiyo imetolewa jana August 19, 2024 na FIFA, baada ya Benchem United kufungua madai dhidi ya Yanga kufuatia kusitisha mkataba wa nyota huyo
Okrah alisajiliwa na Yanga mwezi Januari mwaka huu katika usajili wa dirisha dogo
Hata hivyo nyota huyo hakuwa na wakati mzuri kikosini akisumbuliwa na majeraha ya mara kwa mara pamoja na masuala binafsi ya nje ya uwanja
Yanga imepewa siku 45 kukamilisha malipo ya Benchem United ili kuepuka kifungo cha kutosajili



