Simba - Local - Transfer

Freddy kuibukia USM Alger

Joel JJ By Joel JJ
β€’
21 Aug 2024
Freddy kuibukia USM Alger

Wakati mshambuliaji Leonel Ateba akitua Msimbazi akitokea klabu ya USM Alger, Freddy Michael aliyempisha Mcameroon huyo nae ameelekea USM Alger

Lakini haukuwa usajili wa kubadilishana wachezaji, Simba imetumia zaidi ya Milioni 540 kumn'goa Ateba huku ikifikia makubaliano ya pande mbili kuvunja mkataba wa Freddy ambaye hakukidhi mahitaji ya kocha Fadlu Davies

Tayari Freddy ameondoka nchini kuelekea Algeria kujiunga na USM Alger, mabingwa wa zamani wa kombe la Shirikisho Afrika CAF CC

Freddy atakuwa mchezaji wa tatu kucheza ligi kuu ya Algeria msimu huu akitokea klabu ya Simba

Wachezaji wengine ni Sadio Kanoute na Babacar Sarr waliojiunga na JS Kabylie inayonolewa na kocha wa zamani wa Simba Abdelhak Benchikha

More Stories

Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
3h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
5h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
7h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
9h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
9h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
10h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
12h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
15h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
22h ago
READ MORE β†’
Wapinzani wa Simba, Mighty Wanderers kutua nchini leo wakitokea Malawi
Wapinzani wa Simba, Mighty Wanderers kutua nchini leo wakitokea Malawi
1d ago
READ MORE β†’