Tabora - Local - Simba

Tabora United yaahidi kujisahihisha Ligi Kuu

Joel JJ By Joel JJ
β€’
21 Aug 2024
Tabora United yaahidi kujisahihisha Ligi Kuu

Klabu ya Tabora United, imesema baada ya kufungwa mabao 3-0 dhidi ya Simba Jumapili iliyopita, Uwanja wa KMC Complex uliopo Mwenge, Dar es Salaam, sasa hasira zao wanazielekeza kwa Namungo katika mechi inayofuata

Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Ofisa Habari wa klabu hiyo, Christina Mwagala, alisema wamekubali kuwa wamepoteza mechi kihalali dhidi ya Simba kutokana na sababu mbalimbali ikiwamo ugeni wa wachezaji wengi kwenye kikosi, lakini mchezo huo umewapa mazoezi tosha ya kujua uzito wa mechi za Ligi Kuu

"Tumekubali tumefungwa, lakini tumefunga na timu kubwa ya Simba, kwa hiyo nadhani mechi inayofuata tutapata ushindi kwa sababu hatuchezi tena na mnyama, bali Namungo"

"Mechi iliyopita imetupa mwelekeo na mazoezi tosha ya kujua uzito na mzani wa Ligi Kuu, nadhani sasa wachezaji watakuwa wanaelewa nini wanatakiwa kufanya baada ya mchezo huo," alisema

Mwagala alisema sababu kubwa ya kupoteza mechi hiyo ilikuwa ya kwanza, halafu inacheza na timu kubwa, huku ikiwa na wachezaji wengi wapya

"Tumesajili wachezaji 28 msimu huu, lakini kati ya hao, ni sita tu waliokuwa msimu uliopita, kwa hiyo utaona kuwa 22 wote ni wapya, unakwenda kucheza na timu kama Simba, labda kama tungecheza na timu nyingine, hilo tumemaliza nadhani mechi inayofuata tutawaonesha mashabiki wa soka kuwa Tabora United si timu ya mchezo kama wanavyofikiria," alisema

Kocha Mkuu wa timu hiyo Mkenya, Francis Kimanzi, ameendelea na mazoezi ya kukiunganisha kikosi hicho ambacho kilionekana kukosa muunganiko katika mchezo dhidi ya Simba

Tabora United ipo jijini Dar es Salaam, ikijiandaa na safari ya kwenda mkoani Lindi kucheza mechi ya raundi ya pili ya Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya Namungo, Jumapili ijayo, Uwanja wa Majaliwa, Ruangwa

IPP Media

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
44m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
2h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
4h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’